Thursday 8 January 2009

RUSHWA SOKA LA ITALIA: Bosi wa zamani wa Juventus jela miezi 18!!!

Meneja Mkuu wa zamani wa Klabu kongwe Italia Juventus, Luciano Moggi, amehukumiwa kifungo cha miezi 18 jela baada ya kupatikana na hatia ya rushwa iliyohusu upangaji matokeo wa mechi huko Italia.
Moggi alifungiwa kushiriki kwenye soka huko Italia mwaka 2006 kwa muda wa miaka mitano wakati huo akiwa tayari kiongozi wa Juventus kwa miaka 12.
Mtoto wa Luciano Moggi anaeitwa Alessandro nae amefungwa miezi 14 kuhusiana na kashfa hiyohiyo.
Juventus walivuliwa ubingwa mwaka 2005/6 na kushushwa daraja kuhusiana na kashfa hiyohiyo ya rushwa.
Kwa sasa Juventus wamesharudi daraja la juu liitwalo SERIE A huko Italia.

RATIBA LIGI KUU ENGLAND

Jumamosi, 10 Januari 2009
[saa 9 dak 45 mchana]

Aston Villa v West Brom

[saa 12 jioni]
Arsenal v Bolton
Everton v Hull
Fulham v Blackburn
Middlesbrough v Sunderland
Newcastle v West Ham
Portsmouth v Man City

[saa 2 na nusu usiku]
Stoke v Liverpool

Jumapili, 11 Januari 2009
[saa 10 na nusu jioni]

Wigan v Tottenham

[saa 1 moja usiku]

Man U v Chelsea

Jumatano, 14 January 2009
[saa 5 usiku]

Man U v Wigan

No comments:

Powered By Blogger