Thursday 8 January 2009

Man U yafungwa na Derby kwenye mechi ya kwanza ya Nusu Fainali Carling Cup!!
Ronaldo apata ajali na gari lake la kifahari Ferrari, hakuumia ila gari nyang'anyang'a!
Ferguson adai watashinda mechi ya marudiano na Derby huko Old Trafford!!

Mabingwa Manchester United, wakichezesha kikosi hafifu kwenye Nusu Fainali ya Kombe la Carling walipigwa bao 1-0 na timu hafifu na inayosuasua kwenye Ligi ya daraja la chini ya LIGI KUU, Derby County kwenye mechi iliyofanyika Pride Park uwanjani kwa Derby.
Timu hizi zitarudiana tarehe 20 Januari 2009 huko Old Trafford na mshindi atapambana na mshindi wa Nusu Fainali nyingine iliyochezwa juzi kati ya Tottenham na Burnsley ambako Tottenham alishinda 4-1 uwanjani kwake.
Marudiano kati ya Burnsley na Tottenham ni Januari 21.
Fainali ya Kombe la Carling ni tarehe 1 Machi 2009.
Wakati huohuo, nyota wa Man U, Cristiano Ronaldo, aligongesha gari lake la bei mbaya ya aina ya Ferrari kwenye ukuta wa pembeni wa daraja la chini ya ardhi lakini yeye hakujeruhiwa ila gari liliharibika vibaya.
Ajali hii ilitokea karibu na Uwanja wa Ndege wa Manchester.
Nae Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson amekiri timu yake ilicheza vibaya na ilistahili kufungwa ingawa amesema ni furaha kwao kufungwa goli moja tu kwani katika mechi ya marudiano kazi itakuwa laini kidogo kwani watachezea nyumbani kwao Old Trafford.

No comments:

Powered By Blogger