Wednesday 7 January 2009

CARLING CUP: Tottenham 4 Burnley 1

Tottenham jana waliikung'uta Burnley, timu ya Daraja dogo, mabao 4-1 katika mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la Carling iliyochezwa White Hart Lane nyumbani kwa Tottenham.
Timu hizi zitarudiana Januari 21, nyumbani kwa Burnley.
Leo saa 4 dakika 45 usiku, saa za kibongo, Derby County wanawakaribisha Manchester United kwenye Nusu Fainali nyingine ya Kombe hili.
Mechi ya marudiano ya timu hizi itafanyika Januari 20 huko Old Trafford nyumbani kwa Manchester United.

No comments:

Powered By Blogger