Wednesday 24 December 2008

Ferguson: 'Sinunui Mchezaji Januari!'

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema hawana haja ya kununua Mchezaji yeyote wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa Januari 2009.
Msimu ulipoanza, Manchester United ilinunua Mchezaji mmoja tu ambae ni Dimitar Berbatov waliemnunua kutoka Tottenham kwa Pauni Milioni 30 mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu.
Ferguson ametamka: 'Tulichukuwa Wachezaji 23 kwenda Japan na tumetwaa Ubingwa wa Dunia! Sina wasiwasi kumchezesha yeyote kati ya hao wakati wowote!'

Mourinho anatamani kurudi LIGI KUU ENGLAND!

Aliekuwa Meneja machachari na mwenye vituko wa Chelsea, Jose Mourinho, amekiri ana hamu sana ya kurudi England ili aongoze Klabu ya LIGI KUU.
Mourinho kwa sasa yuko Italia na Timu ya Inter Milan ambayo ndio kinara wa Ligi huko iitwayo Serie A na ambao watakutana na Mabingwa Watetezi wa Ulaya Man U kwenye Raundi ya Mtoano ya UEFA Champions League mwezi Februari mwakani.
Akihojiwa, Mourinho: 'Sifichi. Naipenda LIGI KUU England. Lazima siku moja nirudi huko!'

Scolari ashangazwa na Kadi Nyekundu aliyopewa Nahodha wake John Terry!!

Meneja wa Chelsea Luis Felipe Scolari amesema ameshangazwa na Mwamuzi Phil Dowd kumpa John Terry Kadi Nyekundu.
Terry alipewa kadi hiyo siku ya Jumatatu usiku wakati Chelsea ilipocheza na Everton na Terry kumchezea vibaya Leon Osman kwenye dakika ya 35.
Mara baada ya mechi hiyo Scolari aligoma kufanya mahojiano na Waandishi wa Habari na vilevile alikataza mtu yeyote wa Klabu kuhojiwa.

Fabregas kuepuka kisu!!

Nahodha wa Arsenal Cesc Fabregas alieumizwa goti kwenye mechi kati ya Arsenal na Liverpool amethibitisha kuwa Daktari Bingwa wa mjini Barcelona, Spain ameridhia asifanyiwe upasuaji na badala yake apumzike tu ingawa muda unaokadiriwa goti lake kupona ni miezi minne.

No comments:

Powered By Blogger