Monday 22 December 2008

MABINGWA WA ENGLAND, MABINGWA WA ULAYA na sasa MABINGWA WA DUNIA: Hata Sepp Blatter wa FIFA arukaruka kwa furaha!!!
Baada ya kukabidhiwa Kombe lao na kutawazwa rasmi kuwa wao ndio MABINGWA WA DUNIA, Mabingwa wa England ambao pia ndio Mabingwa wa Ulaya, Manchester United, wakiongozwa na Nahodha wa mechi hiyo, Beki Rio Ferdinand alieshikilia Kombe hilo, waliimba, kupiga kelele, vifijo, nderemo na rapu za kila lugha maana kundi la Wachezaji wa sasa wa Man U wanatoka kila kona ya Dunia!!
Hata Rais wa FIFA Sepp Blatter aliingia uwanjani kwa furaha [pichani juu] maana NI KWELI MAN U NI TIMU YA DUNIA!
Hebu tizama baadhi tu ya Wachezaji: Park ni Mkorea, Vidic anatoka Serbia, Evra ni Mfaransa, Ronaldo na Nani ni Wareno, na ingawa Anderson na Rafael wanatoka Brazil, hawa wawili wanaweza kuongea Kireno pamoja na akina Ronaldo na Nani!
Yupo Tevez toka Argentina, Berbatov wa Bulgaria na usiwasahau Waingereza wenyewe akina Rio, Neville, Carrick, Rooney, Scholes wakisaidiwa na Wajomba zao toka Ireland O'Shea na Evans, na Giggs kutoka Wales!
Alikuwepo chipukizi Danny Welbeck ambae ingawa Mwingereza asili yake ni Ghana!
Na, yupo Manucho toka Angola! Huyu nae anaweza kuteta Kireno na kundi la Ronaldo!
Aaah, yupo Kipa stadi toka Uholanzi Edwin van der Sar, akisaidiwa na Tomasz Kuszczak toka Poland na Chipukizi Ben Amos toka Uingereza!
Juu ya wote, wapo viongozi na hao ni Sir Alex Ferguson anaetoka Scotland na Sir Bobby Charlton ambae ni Mwingereza halisi!
Mbali ya wote, ukiacha kundi la Mashabiki wachache waliotoka Uingereza kuja kuishangilia Man U, ZAIDI YA ASILIMIA 90 YA WATAZAMAJI HAPO UWANJANI YOKOHAMA, JAPAN WALIOKUWA WAKIISHANGILIA MANCHESTER UNITED WALIKUWA NI WAJAPANI HALISI!

No comments:

Powered By Blogger