Tuesday 23 December 2008

IMETHIBITISHWA: Fabregas nje miezi minne!

Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, amethibitisha kuwa Nahodha wake Cesc Fabregas atakuwa nje ya uwanja hadi mwezi Aprili mwakani baada ya Madaktari kugundua ameumia vibaya ndani ya goti lake.

Cesc Fabregas hatihati kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Kiungo mahiri wa Arsenal ambae pia ndie Nahodha, Cesc Fabregas, huenda akawa nje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya kuumia goti kwenye mechi ya Arsenal na Liverpool.
Fagregas aliumia baada ya kupigana kibuyu na Xavi Alonso wa Liverpool katika kipindi cha kwanza na kutolewa nje ya uwanja hapohapo na nafasi yake kuchukuliwa na Vassiriki Diaby.
Hatma yake itajulikana leo baada ya kuchunguzwa na wataalam.

LIGI KUU ENGLAND inaingia patamu!

LIGI KUU ENGLAND sasa inaingia kwenye mechi ngumu na za mfululizo zitakazochezwa kipindi cha Sikukuu ya Krismas siku ya Boxing Day tarehe 26 Desemba 2008 na kufuatiwa na mechi nyingine baada ya mapumziko ya siku moja tu kwa baadhi ya timu.
Kihistoria kipindi hiki ndio hutoa mwanga Timu zipi zitapata mafanikio na zipi zitakumbwa na vita ya kupuruchuka kushushwa daraja.

Kimsimamo, kwa Timu za juu hali iko hivi:

-Liverpool: mechi 18 pointi 39

-Chelsea: mechi 18 pointi 38

-Aston Villa: mechi 18 pointi 34

-Man U: mechi 16 pointi 32

-Arsenal: mechi 18 pointi 31

Ijumaa, 26 Decemba 2008
[saa 9 dak 45 mchana]


Stoke v Man U

[saa 10 jioni]

Liverpool v Bolton
Portsmouth v West Ham
Chelsea v West Brom
Tottenham v Fulham

[saa 12 jioni]

Man City v Hull
Middlesbrough v Everton
Sunderland v Blackburn
Wigan v Newcastle

[saa 2 na robo usiku]

Aston Villa v Arsenal

Jumapili, 28 Decemba 2008
[saa 9 mchana]

Newcastle v Liverpool

[saa 11 jioni]

Arsenal v Portsmouth
Bolton v Wigan
Everton v Sunderland
Fulham v Chelsea
West Brom v Tottenham
West Ham v Stoke
[saa 1 na robo usiku]
Blackburn v Man City

Jumatatu, 29 Decemba 2008
[saa 5 usiku]

Man U v Middlesbrough

Jumanne, 30 Decemba 2008
[saa 5 usiku]

Hull v Aston Villa


No comments:

Powered By Blogger