Sunday 21 December 2008

KLABU BINGWA DUNIANI: Leo Fainali!!!

Liqa de Quito v Manchester United

Leo saa 7 na nusu mchana saa za kibongo, Mabingwa wa Ulaya Manchester United watakutana na Mabingwa wa Marekani ya Kusini Liga de Quito, klabu kutoka Ecuador, katika Fainali ya FIFA CLUB WORLD CUP mechi itakayochezwa Yokohama International Stadium mjini Yokohama huko Japan.
Manchester United iliwahi kuchukua Kombe linalofanana na hili mwaka 1999 pale ilipoifunga Palmeiras ya Brazil iliyokuwa ikiongozwa na Meneja wa sasa wa Chelsea, Luis Felipe Scolari, kwa bao 1-0.
Wakati huo mechi zilikuwa zinashindaniwa na Klabu mbili tu, moja ikiwa Bingwa wa Ulaya na nyingine Bingwa wa Marekani ya Kusini.
Siku hizi mfumo wa Klabu Bingwa Duniani umebadilika na kila Bara la Dunia linawakilishwa na Bingwa wake.
Safari hii, Afrika iliwakilishwa na Al Ahly ya Misri.
Kocha wa Liga de Quito, Edgardo Bauza amesema mechi hii itakuwa ngumu sana lakini watacheza kufa na kupona.
Nae Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson amesema Quito wanacheza kandanda la aina ile ile ya Timu za Marekani ya Kusini na hivyo ni timu ngumu.
Nae Mchezaji Bora wa Ulaya, Cristiano Ronaldo, ametamka; 'Hakika si mechi rahisi lakini nataka kushinda kwa ajili ya timu yangu na mashabiki wa England. Hii itatupa morali tena kushinda Ligi Kuu na Klabu Bingwa Ulaya!'

No comments:

Powered By Blogger