Monday 22 December 2008

Wakati Rooney azawadiwa gari huko Japan, Mashabiki wa Quito walia huko Ecuador!!

Wakati Wayne Rooney, nyota wa Mabingwa wapya wa Dunia Manchester United, akizawadiwa gari mpya aina ya Toyota na kukabidhiwa UFUNGUO MKUBWA WA DHAHABU baada ya kuiwezesha timu yake kunyakua Kombe la Klabu Bingwa Duniani huko Yokohama, Japan baada ya kuiua Liga de Quito kwa bao 1-0, Mashabiki wa Quito waliangua vilio waziwazi huko kwao walipokuwa wakiangalia pambano hilo moja kwa moja toka kwenye TV kubwa zilizowekwa hadharani kwenye mitaa maarufu huko nchini kwao Ecuador!!
Rooney ndie aliechaguliwa Mchezaji Bora wa mechi ya Fainali na pia Mchezaji Bora wa Mashindano hayo yote na vilevile Mfungaji Bora na hivyo kushinda Mpira wa Dhahabu.
Cristiano Ronaldo alizawadiwa Mpira wa Fedha.
Wayne Rooney alifunga jumla ya mabao matatu kwenye Mashindano hayo mawili yakiwa kwenye Nusu Fainali dhidi ya Gamba Osaka ya Japan mechi ambayo Man U walishinda 5-3.

No comments:

Powered By Blogger