Thursday 20 November 2008

HABARI MBALIMBALI ZA LIGI KUU:

Theo Walcott kupasuliwa bega!

Chipukizi wa Arsenal, Theo Walcott, atafanyiwa operesheni ya bega baada ya kuteguka bega hilo juzi katika mazoezi ya kikosi cha Timu ya Taifa ya England kilichokuwa kikijitayarisha kucheza mechi ya kirafiki na Ujerumani.
Theo Walcott ana historia ya kuwa na matatizo ya bega hilo kwani mwaka 2007 alifanyiwa operesheni na kuwekewa pini. Hii majuzi katika mechi ya LIGI KUU dhidi ya Stoke City aliumia tena bega hilohilo.
Inatarajiwa chipukizi huyo atakosa mechi zote za Arsenal kwa mwaka huu 2008.


Benayoun atishia kuhama Liverpool

Myahudi Yossi Benayoun ametishia itabidi ahame Liverpool kwa sababu hapangwi na Meneja Rafa Benitez na badala yake humtumia kwa nadra kama mchezaji wa akiba.
Benayoun alijiunga Lierpool mwaka 2007 akitokea West Ham na mpaka sasa ameshacheza mechi 41 tu nyingi zikiwa kutokea benchi la akiba.

Luka Modric wa Spurs nje wiki 2!

Luka Modric atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki 2 ili kuuguza musuli wa nyonga baada ya kuumia katika mechi Tottenham waliyofungwa na Fulham mabao 2-1 wikiendi iliyokwisha.

No comments:

Powered By Blogger