Saturday 22 November 2008

WAJUE MAREFA WANAOONGOZA KWA KUWAPA WACHEZAJI KADI!!!

Wakati kila timu kwenye LIGI KUU imeshacheza mechi 13 [isipokuwa Man U na Fulham waliocheza 12] jumla ya Marefa 18 ndio waliochezesha mechi zote hizo huku Refa Mike Dean [pichani] aliechezesha jumla ya mechi 11 ndie anaeongoza kwa kutoa kadi nyingi.

Mike Dean ameshatoa Kadi Nyekundu 5 na za Manjano 47.

Anaefuata ni Refa Mike Riley aliechezesha mechi 10 na kugawa Kadi Nyekundu 2 na za Njano 45.

Steve Bennet ana mechi 9 na hajatoa Nyekundu hata moja ingawa amegawa Njano 37.

Rob Styles ana mechi 9, Nyekundu 3 na Njano 33.

Andre Marriner mechi 9, Nyekundu 4 na Njano 32.

Kati ya Marefa hao 18 waliochezesha LIGI KUU mpaka sasa hakuna hata mmoja ambae ametoka uwanjani bila kutoa kadi.

Anaeshika mkia kwa kutoa kadi chache kabisa ni Mark Halsey aliechezesha mechi 6 na kutoa Nyekundu 1 na Njano 6.

No comments:

Powered By Blogger