Saturday 22 November 2008

RIO FERDINAND & ASHLEY COLE WAUNGANA NA RAPA 50 CENT KUTOA FILAMU!

Mastaa wa Uingereza Rio Ferdinand wa Manchester United na Ashley Cole wa Chelsea wamejitosa kwenye utengenezaji filamu baada ya kuchangia dau la kutengeneza filamu iitwayo 'DEAD MAN RUNNING' ambayo itachezwa na mkali wa Rap 50 Cent na Mcheza sinema wa Uingereza aitwaye Danny Dyer.
Filamu hii imeshaanza kutengenezwa huku picha zikichukuliwa mjini London na Manchester.
Katika picha hii Danny Dyer anaekti kama mtu anayedaiwa na kukabwa koo na 50 Cent ili amlipe Pauni laki moja ndani ya masaa 24.
50 Cent ambae ni mwanamuziki mahiri wa kizazi kipya ameshacheza sinema maarufu kama 'Get Rich or Die Tryin' na 'Righteous Kill'.
Rio Ferdinand anamiliki kampuni yake ya kufyatua rekodi iitwayo White Chalk Records na hivi karibuni ilitoa singo yake ya kwanza 'Black Ice' iliyoimbwa na kimwana Nia Jai huku Rio mwenyewe akionekana ndani ya video hiyo.

No comments:

Powered By Blogger