Saturday 22 November 2008

LIGI KUU: Vinara Chelsea & Liverpool wabanwa mbavu, Arsenal apigwa vibaya!!

Vinara wa LIGI KUU Chelsea na Liverpool, wote wakicheza nyumbani kwao, leo wamevutwa jezi na kutoka suluhu na 'timu dhaifu'!!

Chelsea amelezimishwa sare ya 0-0 na Newcastle wakati Liverpool ameenda dro ya 0-0 na Fulham.

Nao Arsenal, ambao wako kwenye mgogoro baada ya kumbwaga chini Nahodha wao William Gallas kufuatia kitendo chake cha kuanika hadharani matatizo ya ndani ya klabu, leo ilishuka City of Manchester Stadium kupambana na timu nyingine inayosuasua, Manchester City, huku Kipa Manuael Almunia akiwa Nahodha.
Arsenal wakajikuta waking'utwa mabao 3-0 katika mechi hii kikiwa kipigo cha pili mfululizo kwa Arsenal baada ya wiki iliyopita kulazwa mabao 2-0 na Aston Villa.
Mabao ya Man City yalifungwa na Stephen Ireland, Robinho na Daniel Sturridge akafunga la 3 kwa penalti baada ya yeye mwenyewe kuchezewa rafu na Beki Johan Djourou.

MATOKEO KAMILI MECHI ZA LEO NI:

Portsmouth 2-2 Hull

Chelsea 0-0 Newcastle

Liverpool 0-0 Fulham

Man City 3-0 Arsenal

Stoke 1-0 West Brom
Middlesbrough 1-3 Bolton

No comments:

Powered By Blogger