Sunday 15 February 2009

DROO YA ROBO FAINALI KOMBE LA FA: Mechi kuchezwa Tarehe 7 na 8 Machi 2009 [Timu inayotajwa kwanza iko nyumbani]

Vigogo watenganishwa!

Blackburn Rovers au Coventry City v Chelsea

Swansea City au Fulham v Manchester United

Cardiff City au Arsenal v Sheffield United au Hull City

Everton v West Ham United au Middlesbrough

KOMBE LA FA: Matokeo

Derby County 1 Man U 4

Everton 3 Aston Villa 1

Everton na Man United zimeingia Robo Fainali ya Kombe la FA baada ya kushinda mechi zao za Raundi ya 5 leo.
Everton alimfunga Aston Villa 3-1 wafungaji wakiwa Jack Rodwell, kijana wa miaka 17 aliepachika bao la kuongoza kwa Everton lakini Villa wakarudisha kwa penalti ya James Milner muda mfupi baadae.
Everton walipata bao la pili kwa penalti kupitia Mikel Arteta na Tim Cahill alipiga msumari wa mwisho kwa goli la tatu.
Manchester United wakicheza ugenini nyumbani kwa Derby County waliibuka na ushindi mzuri wa mabao 4-1.
Mabao ya Man U yalifungwa na Nani, Darron Gibson, Ronaldo na Danny Wellbeck. Bao la Derby lilipatikana kupitia Miles Addison.

No comments:

Powered By Blogger