Tuesday 17 February 2009


KOMBE LA FA: Eduardo arudi uwanjani kwa kishindo, Arsenal 4 Cardiff 0!!!

Mshambuliaji wa Arsenal, Eduardo kutoka Croatia ingawa ni mzaliwa wa Brazil, amerudi uwanjani kuichezea Arsenal kwenye mechi ya marudio Kombe la FA ya Raundi ya 4 mwaka mmoja tangu avunjike vibaya enka [tizama picha siku aliyoumizwa] na ameweza kupachika bao 2 katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Cardiff.

Timu hizi zilitoka sare ya 0-0 katika mechi ya kwanza iliyochezwa nyumbani kwa Cardiff, timu ya daraja la chini.

Mabao mengine ya Arsenal yalifungwa na Robbin van Persie na Bendtner.

Sasa Arsenal atapambana na Burnley kwenye Raundi ya 5 kwake Emirates Machi 7 au 8 na mshindi wa mechi hii atacheza na mshindi wa Sheffield United au Hull City kwenye Robo Fainali.

No comments:

Powered By Blogger