Monday 30 March 2009

Watazamaji wafa mechi ya Ivory Coast na Malawi!!

Katika mechi ya mchujo ya kuingia Fainali Kombe la Dunia 2010 iliyochezwa mjini Abidjan, Ivory Coast kati ya Ivory Coast iliyokuwa ikiongozwa na Didier Drogba, aliepachika bao 2, na Malawi ambapo wenyeji hao waliibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 lakini wamepata majonzi na huzuni kubwa pale Washabiki wao wapatao 19 walipofariki na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa.
Janga hilo lilitokea kabla mechi kuanza pale mashabiki wasiokuwa na tiketi walipotaka kuingia kwa nguvu huku Polisi wakifyatua mabomu ya machozi na ndipo ukuta ukaporomoka na kuleta maafa hayo.
Ingawa janga hilo lilitokea kabla ya mechi, pambano hilo halikuvunjwa na liliendelea kama ilivyopangwa.

MATOKEO MECHI ZA JUMAPILI
AFRIKA:
Mozambique 0 Nigeria o
Ghana 1 Benin o
MAREKANI YA KUSINI:
Ecuador 1 Brazil 1
Peru 1 Chile 3

MECHI ZENYE MVUTO ZA MAKUNDI YA ULAYA ZA MCHUJO WA KUINGIA FAINALI KOMBE LA DUNIA 2010
Jumatano Aprili 1
Denmark v Albania
England v Ukraine
France v Lithuania
Holland v Macedonia
Italy v Republic of Ireland
Turkey v Spain
Wales v Germany

No comments:

Powered By Blogger