Saturday 4 April 2009

Liverpool wachomeka kigoli dakika za majeruhi, waongoza Ligi kwa pointi 2 ingawa Man U ana mechi 2 mkononi!!!!

Kigoli cha babu kilichofungwa na Myahudi Yossi Benayoun dakika ya 92 kimewapa ushindi Liverpool dhidi ya Fulham na hivyo kuwa na pointi 67 huku wamecheza mechi 31.
Mabingwa Man U wanaocheza kesho na Aston Villa uwanjani kwake Old Trafford ni wa pili wakiwa wamecheza mechi 29 na pointi 65 huku Chelsea akifuatia akiwa na pointi 64 kwa mechi 31.
Arsenal ni wa nne kwa mechi 31 na pointi 58.
MECHI ZA JUMAPILI, Aprili 5:
[saa 11 jioni]
Everton v Wigan
[saa 12 jioni]
Man U v Aston Villa

No comments:

Powered By Blogger