Saturday 4 April 2009

Shearer aanza na kipigo nyumbani: Newcastle 0 Chelsea 2!!!!
Adebayor arudi kikosini na kuipa ushindi Arsenal wa 2-0!!!

Nyota wa zamani wa Newcastle, Alan Shearer, alieletwa Newcastle ili kuinusuru kuporomoka daraja leo ameanza kazi kwa kipigo cha 2-0 nyumbani walipofungwa na Chelsea.
Hadi mapumziko jahazi la Newcastle lilikuwa likiselelea vizuri kwa sare ya 0-0 lakini mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Lampard na Malouda yaliwapa ushindi wa bao 2-0 Chelsea na kuwadidimiza chini Newcastle huku wakiwa wamebakiza mechi 7 kujinusuru.
Arsenal, wakiwakaribisha tena nyota wao waliokuwa majeruhi akina Fabregas, Walcott na Adebayor, waliibuka washindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa na Adebayor.
MATOKEO MECHI NYINGINE ZA LEO:
Blackburn Rovers 2 Tottenham 1
Bolton 4 Middlesbrough 1
Hull City 0 Portsmouth o
West Bromwich 0 Stoke City 2
West Ham 2 Sunderland 0

No comments:

Powered By Blogger