Wednesday 1 April 2009

Alan Shearer Bosi mpya Newcastle!!!!

Klabu ya Newcastle ambayo iko nafasi ya tatu toka chini kwenye msimamo wa LIGI KUU England na hivyo kuwamo hatarini kuporomoka daraja imemtangaza Mchezaji wake Nyota wa zamani Alan Shearer kuwa ni Meneja mpya ili kuchukua nafasi ya Joe Kinnear ambae ni mgonjwa.
Newcastle imebakisha mechi nane kwenye LIGI KUU na mechi yao inayofuata na itakayokuwa ya kwanza chini ya Alan Shearer ni Jumamosi dhidi ya Chelsea.

Mido akwaruzana na Zaki!!!

Wachezaji wa Misri, Mido na Zaki, ambao wote wako Klabu moja ya LIGI KUU England, Wigan, wamefarakana wakati wote wakiwa kwenye Timu yao ya Taifa, Misri, ambayo wikiendi iliyopita ilitoka sare 1-1 na Zambia kwenye mechi ya kuwania nafasi Fainali Kombe la Dunia 2010.
Mido ambae alikuwa benchi mechi hiyo amedai Zaki, aliecheza mechi hiyo na kuumia, ametangaza uongo kuwa Kocha wa Misri Hassan Shehata hakumpanga Mido kwa kuwa amegombana nae.
Taarifa hizo zimemuudhi sana Mido na ameibukia vyombo vya habari akimshutumu vikali Zaki

No comments:

Powered By Blogger