Tuesday 7 April 2009

Badala ya Benitez kuzungumzia pambano lake na Chelsea kesho, amvaa Ferguson!!!!!
Gerrard, Drogba wako fiti kuvaana kesho!!!!

Katika hali ya kushangaza, Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, akihojiwa kuhusu pambano la kesho la UEFA CHAMPIONS LEAGUE la Robo Fainali kati ya Liverpool na Chelsea huko Anfield, alimvaa Sir Alex Ferguson na kumuita 'mwoga!'
Wiki iliyopita Sir Alex Ferguson alitamka kuwa Timu itakayobwagwa kati ya Liverpool na Chelsea itabaki ikielekeza macho yake kwenye LIGI KUU England tu na hivyo ndio itakuwa tishio kwa Manchester United.
Wakati huohuo, Steven Gerrard wa Liverpool na Didier Drogba wa Chelsea wametangazwa kuwa fiti kwa mechi hiyo ya kesho baada ya kuwa hatihati kuikosa mechi ya hiyo kwa kuwa majeruhi.
Hata hivyo Liverpool watamkosa Kiungo wao mahiri Javier Mascherano ambae haruhusiwi kucheza baada ya kulambwa Kadi kwenye pambano lao lililopita na Real Madrid.

Wakati Lazio yalalama, Baba wa Nyota Mpya Macheda atetea uamuzi wao wa kuhamia Manchester United

Pasquale Macheda [34], Baba Mzazi wa Kijana wa miaka 17 Federico Macheda alieibuka kuwa Nyota Mpya baada ya kuwapa Manchester United ushindi kwenye mechi yao ya LIGI KUU na Aston Villa ikiwa ni mechi yake ya kwanza kabisa kuichezea, ametetea uamuzi wao wa kifamilia kuhamia Manchester ili kumpa nafasi mtoto wao kuichezea Manchester United.
Baada ya Macheda kuibuka kuwa lulu siku ya Jumapili, Klabu ya Lazio ilinung'unika kwa kumpoteza Macheda aliekuwa Mchezaji wao kwenye Timu yao ya Vijana.
Rais wa Lazio, Claudio Lotito, aliitaka Italia ibadilishe sheria zake inayozuia Vijana wa chini ya miaka 18 kusaini mkataba na Klabu.
Manchester United ilimnyakua Macheda kutoka Lazio Septemba 2007 wakati akiwa na miaka 16 na kumsainisha mkataba wa kuwa Mchezaji mwanafunzi kwenye Chuo chao cha Soka.
Macheda alisaini mkataba kamili Mwaka jana, mwezi Agosti, alipotimiza miaka 17, wa kuwa Mchezaji wa Kulipwa wa Man U na akaingizwa kwenye Timu ya Akiba.
Baba huyo wa Nyota Macheda anasema: 'Tunaishkuru Lazio kwa kumfunza vyema. Ilikuwa ngumu kuikataa ofa ya Manchester United.'
Baba huyo alihangaika sana wakati akiwa Italia ili kumpa nafasi mwanawe Federico Macheda nafasi ya kuendeleza ndoto yake ya kuwa Staa wa Soka.
Ilibidi afanye kazi zaidi ya mbili kwa siku, sokoni na nyingine usiku kucha, ili kugharamia ndoto ya mwanawe, na kuendesha gari kwa saa zaidi ya moja ili kumfikisha mwanawe Uwanja wa Lazio kwa mazoezi na baadae kwenda kumchukua baada ya mazoezi.
Macheda aliposaini na Manchester United mwaka 2007, familia yake ikahamia Manchester na kupewa nyumba jirani na Uwanja wa Carrington ambako Man U hufanyia mazoezi.
Siku ya mechi ya juzi na Aston Villa, Pasquale Macheda, mkewe Loredana na Simone, mtoto wao wa kiume, mdogo wa Federico, walikuwepo Old Trafford wakishuhudia historia ikiwekwa.
Baada ya kufunga bao hilo la ushindi, Federico alikimbia hadi walipoketi familia yake na kumkumbatia Baba yake aliyekuwa akilia kwa furaha.
Kitendo hicho cha kutoka nje ya uwanja kilimafanya Macheda apewe Kadi ya Njano na Refa Mike Riley.
Ingawa Lazio wanalalamika kupokonywa Macheda, mtu pekee aliyekuwa na furaha kwa mafanikio ya Kijana huyo ni Kocha wake wa zamani wa Timu ya Vijana hapo Lazio, Stefano Avincola, aliesema: 'Nimefurahi sana kwa ajili yake! Tulijaribu kuwashawishi abaki Lazio lakini tunaelewa nini kimewapeleka Man U. Familia ya Macheda ni waungwana kwani walikuja kutushkuru kwa kumlea vizuri Federico.'

No comments:

Powered By Blogger