Monday 6 April 2009

ULAYA kuwaka moto kesho na Jumatano!!

UEFA CHAMPIONS LEAGUE inaingia hatua ya Robo Fainali hapo kesho usiku na Jumatano.

Kesho Jumanne, saa 3 dakika 45 usiku, Villareal ya Spain watakuwa wenyeji wa Arsenal ambayo itakuwa na pengo kubwa la kumkosa Mshambuliaji wao wa kutegemewa Robin van Persie ambae ni majeruhi.
Nao Mabingwa Watetezi wa Kombe hili, Manchester United, watakuwa nyumbani Old Trafford wakiikaribisha Klabu ya Ureno FC Porto na watawakosa Rio Ferdinand na Dimitar Berbatov walioumia lakini Wachezaji wengine ambao hawakucheza mechi ya jana ya ushindi dhidi ya Aston Villa kina Wayne Rooney, Nemanja Vidic, Paul Scholes na Park wote wamo kwenye Kikosi.
Jumatano usiku, pia saa 3 dakika 45, bongo taimu, kutakuwa na mechi zinazotegemewa kuwa na patashika kubwa pale Barcelona watakapoikaribisha Bayern Munich na nyingine ni ile vita ya Timu za England wakati Liverpool, wakiwa nyumbani Anfield, watakapomenyana na Chelsea ambayo itakuwa na muuaji wao hatari Didier Drogba alieikosa mechi ya LIGI KUU Jumamosi dhidi ya Manchester City kwa kuwa na maumivu.
Mechi hizi zitarudiwa wiki ijayo.

No comments:

Powered By Blogger