Saturday 11 April 2009

REFA ADAI KABLA YA MECHI CHELSEA WALIMTAKA ASIWAPE KADI WACHEZAJI WAO!!!

Refa kutoka Denmark, Claus Bo Larsena, aliechezesha pambano la Jumatano iliyopita huko Anfield kati ya Liverpool na Chelsea la Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE ambalo Chelsea ilishinda mabao 3-1, amedai kwenye Kikao cha kujadili usalama kabla ya mechi hiyo kilichohudhuriwa na Maofisa toka UEFA, Chelsea, Liverpool, Polisi na Waamuzi wa pambano hilo, alistushwa sana pale Afisa mmoja wa Chelsea kumwambia bila kificho 'hawakaribishi ' Wachezaji wao kupewa Kadi za Njano na hivyo kukosa mechi ya marudiano huko Stamford Bridge siku ya Jumanne. Hata hivyo kwenye mechi hiyo Refa Claus Bo Larsen alimtwanga Nahodha wa Chelsea, John Terry, Kadi ya Njano na hivyo ataikosa mechi ya Jumanne.
Wengine wa Chelsea waliokuwa hatarini kuikosa mechi hiyo ya Jumanne endapo wangepata Kadi ni Anelka na Ashley Cole lakini bahati nzuri waliepuka Kadi.
'Sijawahi kuona kitendo kama hicho!' Refa Claus Bo Larsen alisema 'Nimeshawahi kuhudhuria vikao vya aina hivyo zaidi ya 100, haijatokea! Lakini niliwaambia palepale Mchezaji akifanya kosa la Kadi ya Njano basi lazima nitampa Kadi!!'

No comments:

Powered By Blogger