Thursday 9 April 2009

MATOKEO: Duru la kwanza Robo Fainali UEFA CUP
Hamburg 3-1 Manchester City
PSG 0-0 Dynamo Kiev
Shakhtar Donetsk 2-0 Marseille
Werder Bremen 3-1 Udinese
Marudiano ni wiki ijayo tarehe 16 Aprili 2009.

Gallas kukosa mechi zilizobaki msimu huu!

Beki wa Arsenal, William Gallas, atazikosa mechi zote zilizobaki msimu huu baada ya kuumia goti kwenye mechi ya dro ya 1-1 na Villareal ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Habari hizi zimethibitishwa na Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal.

Gerrard kufanyiwa uchunguzi maumivu yake ya nyonga!

Nahodha na nguzo kubwa ya Liverpool, Steven Gerrard, atafanyiwa uchunguzi baada ya kuumia kwenye mechi waliyofungwa na Chelsea mabao 3-1 kwenye kinyang'anyiro cha UEFA CHAMPIONS LEAGUE na kuna wasiwasi mkubwa huenda akazikosa mechi muhimu zijazo.
Jumamosi, Liverpool wanapambana na Blackburn kwenye mechi muhimu ya LIGI KUU England na Jumanne ijayo wanarudiana na Chelsea kwenye mpambano wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Vidic akiri: 'Tulijisahau!'

Beki wa Mabingwa, Manchester United, Nemanja Vidic, amekiri mwendo mbovu wa Mabingwa hao katika mechi za hivi karibuni umetokana na wao wenyewe kulewa ushindi na kuzichukulia mechi zao kama kitu rahisi hasa watu walipoanza kuwasifu kuwa wana uwezo mkubwa wa kutwaa Mataji matano msimu baada ya tayari kuyatwaa yale ya Ubingwa wa Dunia na Kombe la Carling huku wakiwa kwenye nafasi nzuri kuutwaa Ubingwa wa LIGI KUU, kunyakua Kombe la FA na kuliteka tena Kombe la UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Man U hivi karibuni walifungwa mechi mbili mfululizo kwenye LIGI KUU, walipigwa na Liverpool 4-1 na Fulham 2-1, kisha wakaokolewa na mtoto wa miaka 17 Federico Macheda alipowapa ushindi wa 3-2 dhidi ya Aston Villa.
Juzi walilazimishwa sare ya 2-2 na FC Porto kwao Old Trafford kwenye mpambano wa duru la kwanza la UEFA CHAMPIONS LEAGUE na sasa Mabingwa hao ama inabidi washinde huko Porto au watoke sare ya zaidi ya bao 2-2 ili waingie Nusu Fainali.

MECHI ZA WIKIENDI ZA LIGI KUU ENGLAND:
Jumamosi, Aprili 11
[saa 8:45 mchana]
Liverpool v Blackburn
[saa 11 jioni]
Chelsea v Bolton
Middlesbrough v Hull City
Portsmouth v West Brom
Sunderland v Man U
Tottenham v West Ham
Wigan v Arsenal
[saa 1:30 usiku]
Stoke City v Newcastle
Jumapili, Aprili 12
[saa 10 jioni]
Aston Villa v Everton
[saa 12;10 jioni]
Man City v Fulham

No comments:

Powered By Blogger