Saturday 11 April 2009

Federico 'Kiko' Macheda awapa ushindi tena Man U!!!

Kijana wa miaka 17, Federico Macheda, aka Kiko, kwa mara ya pili mfululizo ameifungia Manchester United bao la ushindi baada ya kuingizwa kipindi cha pili dakika ya 74 kumbadilisha Berbatov na ilimchukua sekunde 46 tangu aingie kufunga bao la pili lililowapa Man U ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya Sunderland.
Wiki iliyopita Macheda alifunga bao la 3 na la ushindi kwenye dakika za majeruhi Man U walipoifunga Aston Villa 3-2.
Man U wamerudi tena kileleni mwa LIGI KUU England baada ya uongozi kuchukuliwa na Liverpool kwa masaa kadhaa wakati Liverpool walipoishindilia Blackburn mabao 4-0 kwenye mechi iliyoaanza mapema leo.


MATOKEO MECHI ZINGINE ZA LEO NI:
Chelsea 4 Bolton 3
Middlesbrough 3 Hull 1
Portsmouth 2 West Brom 2
Tottenham 1 West Ham 0
Wigan 1 Arsenal 4
Liverpool 4 Blackburn 0

No comments:

Powered By Blogger