Sunday 12 April 2009

LIGI KUU LEO Jumapili Aprili 12:

[saa 10 jioni kibongo]

Aston Villa v Everton

[saa 12 dakika 10 kibongo]


Man City v Fulham


Ferguson amsifu Bwana Mudogo Federico Macheda aka Kiko!!!!!

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amemsifu chipukizi wao wa miaka 17 mzawa wa Italia, Federico Macheda, maarufu kama 'Kiko', baada ya mara ya pili mfululizo, ndani ya siku sita tu, akitoka benchi na kuingia uwanjani na kuipa ushindi Man U.

Jana aliingizwa kumbadilisha Berbatov katika dakika ya 74 huku mechi ikiwa Sunderland 1 Man U 1 na baada ya sekunde 46 tu ukiwa ndio mpira wake wa kwanza kuugusa akaipatia Man U bao la pili na la ushindi.
Wiki iliyopita aliingizwa kipindi cha pili na katika dakika za majeruhi huku mechi ikiwa Man U 2 Aston Villa 2, akapachika bao la 3 na la ushindi.
Katika mechi zote hizo mbili, kama matokeo yangebaki suluhu, basi Liverpool angenyakua uongozi wa LIGI KUU England lakini ushujaa wa Macheda aka Kiko umehakikisha Man U anaendelea kuongoza ligi.
Sir Alex Ferguson amesema: 'Huyu kijana ana kitu spesho!! Nilipomwingiza sikumpa maelekezo yeyote maalum! Nilimwambia tu ingia na cheza!!'

No comments:

Powered By Blogger