Friday 17 April 2009

Man City watupwa nje UEFA CUP!!!!!

Manchester City, mbali ya kuwafunga Hamburg ya Ujerummani kwa bao 2-1 hapo jana, walijikuta wakitolewa nje ya Kombe la UEFA kwani katika mechi ya kwanza iliyochezwa huko Ujerumani wiki iliyopita walifungwa mabao 3-1. Hivyo Man City wameyaaga mashindano hayo kwa kufungwa jumla ya mabao 4-3. Sasa Hamburg wanaingia Nusu Fainali na watakumbana na Wajerumani wenzao Werder Bremen.

MATOKEO MECHI NYINGINE ZA ROBO FAINALI ZA JANA:

Dynamo Kiev 3 PSG 0 [Kiev anasonga mbele kwa jumla ya mabao 3-0]

Udinese 3 Werder Bremen 3 [Werder Bremen mshindi kwa jumla ya mabao 6-4]


Marseille 1 Shakhtar Donetsk 2 [Shakhtar Donetsk mshindi kwa bao 4-1]


NUSU FAINALI:

30 Aprili 2009
Dynamo Kiev v Shakhtar Donetsk
Hamburg v Werder Bremen


MARUDIO NI TAREHE 7 MEI 2009


FAINALI TAREHE 20 MEI 2009

No comments:

Powered By Blogger