Wednesday 15 April 2009

Cristiano Ronaldo awaua Wareno wenzake!!!

Goli linalostahili kufungwa na Mchezaji Bora Duniani lilifungwa na Mchezaji Bora Duniani pale Cristiano Ronaldo alipopiga shuti la umbali wa kama mita 30 kwenye dakika ya 5 na kuipa Timu yake Manchester United ushindi ugenini.
Haijatokea hata siku moja Timu yeyote ya Uingereza kushinda Ureno.
Manchester United, wakiwa na Mchezaji Bora Duniani Ronaldo, walihitaji ushindi ili waingie Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na waliupata ushindi na kutawala mechi yote.

Arsenal Waingia Nusu Fainali kwa kishindo!

Arsenal, wakiwa kwao Emirates Stadium, wamepata ushindi wa kishindo wa bao 3-0 dhidi ya Villareal na sasa watakutana na Mabingwa Watetezi wa Ulaya Manchester United kwenye Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Nusu Fainali nyingine itawakutanisha Chelsea na Barcelona.

RATIBA NI:

28 APRILI 2009

Barcelona v Chelsea

29 APRILI 2009

Man U v Arsenal

5 MEI 2009

Arsenal v Man U

6 MEI 2009

Chelsea v Barcelona

No comments:

Powered By Blogger