Saturday 18 April 2009

Ferguson amuunga mkono Allardyce kumshutumu Benitez!!!! Wamwita 'kiburi' na mwenye 'dharau' kubwa!!!!

Meneja wa Blackburn Rovers, Sam Allardyce, ametoa shutuma kali kuhusiana na vitendo vya Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, ambae alinaswa na kamera kwenya mechi kati ya Liverpool na Blackburn ya wiki iliyopita ambayo Liverpool walishinda 4-0 akitoa ishara za mikono kwenye dakika ya 33 mara baada ya Fernando Torres kufunga bao la pili kuashiria Blackburn 'wamekwisha'!!!

'Ni dharau kubwa kwangu na Timu yote ya Blackburn!' Sam Allardyce alidai. 'Inasikitisha na kukera! Ndio tulifungwa na Timu Bora Liverpool lakini kufanya kitendo kile ni dharau kubwa sana!
Allardyce alisema baada ya mechi hiyo iliyochezwa Anfield nyumbani kwa Liverpool alikwenda kwenye ukumbi wa Klabu hiyo ili apate mvinyo na Benitez kama ilivyo desturi kwenye LIGI KUU England kuwa Mameneja hukutana baada ya mechi lakini Benitez hakutokea na badala yake msaidizi wake Sammy Lee ndie alikuwepo.
Allardyce akazidi kusikitika: 'Hakutokea na hakujali hata kutuma ujumbe kwa nini hakuwepo wakati yeye ndio mwenyeji! Hii inadhihirisha yeye ni mtu wa aina gani!!'
Nae Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, ambae siku za hivi karibuni amekuwa akiandamwa na mashambulizi kutoka kwa Benitez, amemuunga mkono Sam Allardyce.
Ferguson alimponda Benitez kwa kusema: 'Huyu Benitez ameiita Everton ambayo tunacheza nayo Wembley Jumapili Nusu Fainali ya FA Cup 'klabu ndogo'!! Everton ni timu kubwa!!! Hiki ni kiburi!! Lakini huwezi kuisamehe dharau!! Walipowafunga Blackburn bao la pili zile ishara zake ni dharau kubwa!! Sidhani Sam Allardyce anastahili kufanyiwa vitendo hivyo!! Allardyce amefanya mambo makubwa kwenye LMA [League Managers Association: Chama cha Mameneja wa Ligi]'

Moyes wa Everton astuka uteuzi wa Refa Mike Riley kuchezesha Nusu Fainali ya FA CUP dhidi ya Man U!!!

Meneja wa Everton, David Moyes, ambayo klabu yake inashuka Wembley Jumapili kupambana na Manchester United kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA, amehoji uteuzi wa Refa Mike Riley kuchezesha pambano hilo.
Awali Refa Steve Bennet ndie alipangwa kuwa Mwamuzi laki ikabidi ajitoe kwa kuwa ni mgonjwa na uteuzi wa Mike Riley haukumfurahisha David Moyes ambae ashawahi kumlaumu Riley kwa kuipendelea Man U pale mwaka 2003 kwenye mechi ya mwisho kabisa ya LIGI KUU alipoipa Man U penalti iliyoiua Everton na kuwakosesha nafasi ya kucheza UEFA CUP msimu uliofuata.
Moyes anasema: 'Kuna Mwandishi alinihoji ikiwa mie nadhani Mike Riley ni shabiki wa Man U, nadhani ikiwa ni hivyo basi ni jukumu la FA kushughulikia hilo.'
FA, Chama cha Soka England, kimejibu hoja hizo kwa kutamka Marefa wao wote ni wakweli, hawapendelei na huchezesha kwa haki.
Walisema: 'Mike Riley ni mmoja wa Maarefa wetu wazoefu na wenye uwezo mkubwa. Tuna hakika Jumapili atafanya kazi nzuri'

KESI YA KUTEMA MATE: Fabregas atoa utetezi wake kwa FA

Nahodha wa Arsenal, Cesc Fabregas, amewasilisha utetezi wake kwa FA, Chama cha Soka cha England, kufuatia tuhuma kutoka Klabu ya Hull City kuwa alimtemea mate Meneja Msaidizi wa Hull, Brian Horton hapo Machi 17 mara baada ya mechi ya FA Cup kati ya Arsenal na Hull ambayo Arsenal walishinda 2-1. Siku hiyo Cesc Fabregas hakucheza kwa kuwa alikuwa majeruhi na ingawa alivaa kiraia alikuwepo kwenye benchi la Timu ya Arsenal.
Brian Horton na Kocha wa viungo wa Hull, Sean Rush, tayari washapeleka ushahidi wao.
FA imekiri kupokea makabrasha yote na wameahidi kutangaza nini kitafuatia hivi karibuni.

LEO NI:
Jumamosi, 18 Aprili 2009 [saa za kibongo]
LIGI KUU ENGLAND
[saa 11 jioni]
Aston Villa v West Ham
Middlesbrough v Fulham
Portsmouth v Bolton
Stoke v Blackburn
Sunderland v Hull City
FA CUP NUSU FAINALI
[saa 1 na robo usiku]
Arsenal v Chelsea

Klabu ya Macedonia FK Pobeda yafungiwa miaka 8 na UEFA kwa kupanga matokeo!!! Rais wake na Mchezaji mmoja wala kifungo cha maisha!!!!

UEFA imeifungia Klabu ya Macedonia, FK Pobeda, kwa miaka minane kutoshiriki mashindano yeyote ya UEFA kwa kupatikana na hatia ya kupanga matokeo kwenye mechi zilizochezwa Julai 13 na 21 mwaka 2004 dhidi ya FC Pyunit za UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

UEFA vilevile imemfungia Rais wa Klabu hiyo na Mchezaji wake mmoja maisha. Pia UEFA imeiomba FIFA ihalalishe adhabu zote hizi kuwa za dunia nzima.

No comments:

Powered By Blogger