Wednesday 15 April 2009

Piga, nikupige ya Chelsea na Liverpool yaishia Liverpool chaliiiiiii!!!!!!

Ndani ya ngome yao, uwanjani Stamford Bridge huku wakicheza bila Nahodha wao John Terry aliekuwa na Kadi, Chelsea waliweza kuulinda ushindi wao wa 3-1 walioupata nyumbani kwa Liverpool, Anfield wiki iliyopita, kwa kuweza kutoka suluhu ya mabao 4-4 na hivyo kusonga mbele kuingia Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE kwa jumla ya mabao 7-5 na sasa watapambana na timu ngumu Barcelona ambao jana walitoka dro ya 1-1 na Bayern Munich na hivyo pia kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5-1 baada ya kuishinda Bayern Munich 4-0 kwenye mechi ya kwanza. Liverpool, wakicheza bila ya Nahodha wao Steven Gerrard ambae ni majeruhi, waliongoza 2-0 kwa mabao yaliyofungwa na Aurelio dakika ya 19 na lile la penalti ya Alonso dakika ya 28.
Kipindi cha pili mabao ya Drogba dakika ya 52 na Alex dakika ya 57 yaliwafanya Chelsea wasawazishe na dakika ya 76 Lampard akawapa uongozi wa mabao 3-2.
Liverpool wakaibuka na kusawazisha kupitia Lucas [81] na dakika moja baadae Kuyt akawafungia bao la 4 na kuwafanya Liverpool wahitaji bao moja tu ili waingie Nusu Fainali huku mechi ikiwa imebakiza dakika 8 kwisha.
Lakini Frank Lampard akawagalagaza aliposawazisha dakika ya 89 na mechi ya piga nikupige ikaisha kwa mabao 4-4 huku Chelsea wakitoka kidedea kwa kuingia Nusu Fainali.

Leo ni zamu ya Man U huko Ureno na Arsenal nyumbani Emirates Stadium.


Leo usiku Man U, Mabingwa watetezi wa Kombe hili la UEFA CHAMPIONS LEAGUE wanashuka Estadio do Dragao kutafuta ushindi au angalau suluhu ya 3-3 ili waingie Nusu Fainali wataporudiana na wenyeji wao FC Porto ya Ureno.
Katika mechi ya kwanza huko Old Trafford, Timu hizi zilitoka suluhu 2-2.
Man U wameongezewa nguvu baada ya kutangazwa Mlinzi wao mahiri Rio Ferdinand ambae hajacheza mechi kadhaa kwa kuwa alikuwa majeruhi sasa yuko fiti na leo ataingia dimbani.
Nao Arsenal, wakiwa nyumbani Emirates Stadium, wana nafasi nzuri ya kusonga mbele hasa baada ya kutoka suluhu ugenini ya bao 1-1 na Villareal huko Spain wiki iliyopita.
Arsenal, ingawa watawakosa Johan Djourou, Gael Clichy na William Gallas walioumia, watanufaika sana kwani Villareal wataikosa injini yao ya kwenye kiungo Marcos Senna ambae ameumia na ambae ndie alikuwa Mfungaji wa bao la Villareal timu hizi zilipocheza wiki iliyopita
.

No comments:

Powered By Blogger