Saturday 18 April 2009

Wolverhamton yapanda daraja na kuingia LIGI KUU England msimu ujao!!

Wolverhampton leo imeifunga QPR bao 1-0 na kujihakikishia Ubingwa wa Daraja la Championship lililo chini tu ya LIGI KUU na pia kuwa Timu ya kwanza kutoka Daraja hilo kupanda kuingia LIGI KUU msimu ujao huku zimebaki mechi mbili ili msimu umalizike. Timu 3 toka Daraja hilo hupanda na tatu kutoka LIGI KUU huporomoka kila msimu. Mara ya mwisho Wolverhampton, au Wolves kama wanavyojulikana kwa kifupi, kuchezea LIGI KUU ilikuwa mwaka 2004.

MATOKEO LIGI KUU England leo:
Aston Villa 1-1 West Ham
Middlesbrough 0-0 Fulham
Portsmouth 1-0 Bolton
Stoke 1-0 Blackburn
Sunderland 1-0 Hull

No comments:

Powered By Blogger