Saturday 18 April 2009

Arsenal v Chelsea

Leo saa moja na robo saa za bongo, Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la FA itachezwa mjini London Uwanja wa Wembley kati ya Arsenal na Chelsea.
Nusu Fainali ya pili itachezwa kesho kati ya Manchester United na Everton pia Uwanjani Wembley.
Fainali ya Kombe hili la FA itafanyika Wembley tarehe 30 Mei 2009.
Timu zote zinakabiliwa na majeruhi kadhaa huku Arsenal wanaonekana wameathirika zaidi kwani watawakosa Kipa Almunia, Sagna, Clichy, Gibbs na Gallas.
Chelsea nao watamkosa Deco ingawa Nahodha wao John Terry anategemewa kuwepo Uwanjani baada ya kuikosa mechi ya juzi na Liverpool ambayo hakucheza kwa kuwa na Kadi. Mchezaji wao mlinzi wa pembeni, Jose Bosingwa, huenda akawepo baada ya kupona maumivu yaliyomkosesha mechi kadhaa.
Vikosi vinatumainiwa kutokana na:
Arsenal: Fabianski, Eboue, Toure, Silvestre, Gibbs, Arshavin, Song, Fabregas, Walcott, Adebayor, Van Persie, Mannone, Nasri, Diaby, Bendtner, Vela, Eduardo, Denilson, Ramsey.
Chelsea: Cech, Hilario, Belletti, Alex, Ivanovic, Carvalho, Terry, Mancienne, A Cole, Lampard, Ballack, Obi, Kalou, Essien, Malouda, Di Santo, Anelka, Quaresma, Stoch, Drogba
Refa atakuwa: Martin Atkinson

No comments:

Powered By Blogger