Wednesday 15 April 2009

Ferguson: 'Leo Wachezaji lazma waukumbuke ule moto wa 1999!!!'

Wenger: 'Hatuchezi tupate sare leo, tutacheza kutafuta ushindi tu!!!'


Sir Alex Ferguson amewataka Wachezaji wa Manchester United waikumbuke ari na moyo wa ile Timu yake ya mwaka 1999 [pichani] wakati leo wanapoingia Uwanja wa FC Porto uitwao Estadio do Dragao ambao hakuna hata Timu moja toka England iliyowahi kucheza hapo, zikiwamo Arsenal, Liverpool, Chelsea na Man U wenyewe, na kutoka na ushindi. Man U, baada ya kutoka sare 2-2 na FC Porto huko Old Trafford wiki iliyopita, wanahitaji ushindi au sare ya zaidi ya 2-2 ili wasonge mbele na kuingia Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Mwaka 1999, Man U ilitoka sare na Juventus Uwanjani kwake Old Trafford na katika mechi ya marudiano huko Turin, Italia ikajikuta iko nyuma kwa bao 2-0 lakini wakiongozwa na Nahodha wao Roy Keane waliibuka kwenye mechi hiyo washindi kwa bao 3-2 na wakaendelea mpaka Fainali ambayo walikuwa nyuma ya Bayern Munich kwa bao 1-0 lakini wakashinda kwenye dakika za majeruhi kwa bao 2-1 na kuwa Mabingwa wa Ulaya [pichani wakiwa na Kombe].
Ferguson anasema: 'Naiamini Timu yangu na naamini tunaweza kucheza kwa juhudi na moyo kama ule wa mwaka 1999!'
FC Porto ambao ndio wenyeji leo watacheza mechi hii huku wakiwa na dosari kubwa baada ya UEFA kuthibitisha kuwa Meneja wa FC Porto, Jesualdo Ferreira, kufungiwa mechi moja na hivyo haruhusiwi kukaa benchi la akiba.
Ferreira amefungiwa baada ya kupatikana na hatia ya kumkashifu Refa kwenye mechi ya nyuma ya mashindano haya wakati Porto ikicheza na Atletico Madrid hapo Februari 24.
Arsenal ambao walitoka suluhu ya 1-1 huko Spain walipocheza na Villareal, leo Uwanjani kwao Emirates wanahitaji sare ya 0-0 ili wasonge mbele lakini Meneja wao, Arsene Wenger, amesema wao siku zote wanacheza kushinda tu na ukitafuta suluhu basi unakaribisha maafa!!
Ingawa Arsenal wana majeruhi wengi wakiwemo Kipa Almunia, Gallas, Clichy na Djourou, Wenger bado anaamini Chipukizi wake watashinda tu.
Wenger anadai: 'Vijana wangu ni washindi!! Hatukati tama! Hata kwenye ligi ingawa tuko nyuma sana lakini bado tuna imani!!'


Wachezaji wa Man U wamejaa kwenye listi ya Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka anaechaguliwa na Chama cha Wachezaji wa Kulipwa [PFA]!!!!


Katika Listi ya mwisho ya Wachezaji watakaopigiwa kura na Chama cha Wachezaji wa Kulipwa huko England [PFA yaani Professional Footballers Association] kuteua Mchezaji Bora wa mwaka wapo Wachezaji Watano kutoka kwa Mabingwa Manchester United. Wachezaji hao ni Rio Ferdinand, Ryan Giggs, Cristiano Ronaldo, Edwin van der Sar na Nemanja Vidic.
Mchezaji pekee ambae yumo kwenye listi hiyo na hatoki Man U ni Steven Gerrard wa Liverpool.
Uteuzi na Tuzo yenyewe hiyo zitatolewa Aprili 26.
Wale waliomo kwenye listi ya mwisho kugombea Tuzo ya Mchezaji Chipukizi wa mwaka ni Gabriel Agbonlahor [Aston Villa], Rafael Da Silva [Man U], Jonny Evans [Man U], Stephen Ireland [Man City], Aaron Lennon [Tottenham] na Ashley Young [Aston Villa].

No comments:

Powered By Blogger