Thursday 9 April 2009

Liverpool yatolewa utumbo nyumbani Anfield: Liverpool 1 Chelsea 3

Wakiwa nyumbani Anfiled, Liverpool wamejikuta mguu mmoja nje ya kutolewa UEFA CHAMPIONS LEAGUE baada ya kupigwa bao 3-1 na Chelsea.
Marudiano ya timu hizi ni Jumanne ijayo Aprili 14 huko Stamford Bridge kwenye ngome ya Chelsea.
Fernando Torres aliwapa furaha Liverpool dakika ya 6 ya mechi alipofunga bao.
Lakini shujaa asiyetegemewa aliibuka kwa upande wa Chelsea pale Mlinzi Branislav Ivanovic aliposawazisha kwa kichwa dakika ya 39 na kupachika la pili dakika ya 62 kwa kichwa tena.
Kisha Didier Drogba akaweka msumari wa mwisho kwa kufunga bao la 3 dakika ya 67.
Chelsea walipata pigo kwenye mechi hii wakati Nahodha wao John Terry alipopewa Kadi ya Njano na hivyo kumaanisha hawezi kucheza mechi ya marudiano ya wiki ijayo.
Liverpool: Reina, Arbeloa, Carragher, Skrtel, Aurelio (Dossena 75), Kuyt, Lucas (Babel 79), Alonso, Riera (Benayoun 67), Gerrard, Torres.
Akiba hawakucheza: Cavalieri, Hyypia, Agger, Ngog.
Kadi: Aurelio.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Terry, Alex, Ashley Cole, Kalou, Ballack, Essien, Lampard, Malouda, Drogba (Anelka 79).
Akiba hawakucheza: Hilario, Carvalho, Belletti, Mancienne, Mikel, Deco.
Kadi: Kalou, Terry.
Watazamaji: 42,543
Refa: Claus Bo Larsen (Denmark).

Barcelona watamu!!!!!
Waichabanga Bayern Munich 4-0!!!!
Ndani ya Uwanja wao Nou Camp, Barcelona waliwapiga bila huruma Bayern Munich 4-0 huku wakicheza soka tamu sana.
Mabao ya Barcelona yalifungwa na Lionel Messi, mabao mawili, Samuel Eto'o na Thierry Henry.
Timu hizi zitarudiana Jumanne ijayo huko Ujerumani.
Vikosi vilikuwa:
Barcelona: Valdes, Dani Alves, Marquez, Pique, Puyol, Xavi, Toure Yaya (Busquets 81), Iniesta, Messi, Eto'o (Bojan 89), Henry (Keita 74).
Akiba hawakucheza: Pinto, Caceres, Gudjohnsen, Sylvinho.
Kadi: Messi, Marquez.
Magoli: Messi 9, Eto'o 12, Messi 38, Henry 43.
Bayern Munich: Butt, Oddo, Demichelis, Breno, Lell, Altintop (Ottl 46), Schweinsteiger, Van Bommel, Ze Roberto (Sosa 76), Ribery, Toni.
Akiba hawakucheza: Rensing, Podolski, Lahm, Borowski, Badstuber.
Kadi: Lell, Demichelis.
Watazamaji: 97,000
Refa: Howard Webb (England).

LEO ROBO FAINALI UEFA CUP: Hamburg v Man City

Timu pekee toka England iliyobaki kwenye UEFA CUP ni Man City na leo ipo ugenini huko Ujerumani ikipambana kwenye mechi ya kwanza ya Robo Fainali na Timu ya Ujerumani Hamburg.
Marudio ya mechi hii yatafanyika wiki ijayo nyumbani kwa Man City, City of Manchester Stadium, tarehe 16 Aprili.
Mechi nyingine za duru la kwanza la Robo Fainali ni:
PSG v Dynamo Kiev
Shakhtar Donetsk v Marseille
Werder Bremen v Udinese

No comments:

Powered By Blogger