Wednesday 8 April 2009

Man U wabanwa kwao kwa sare ya 2-2, Arsenal wanufaika ugenini kwa sare ya 1-1!!!

Mabingwa watetezi wa Ulaya, Manchester United, wakicheza soka bovu kabisa nyumbani Ol Trafford wametoka suluhu 2-2 na FC Porto ya Ureno.
Man U sasa lazima washinde mechi ya marudiano huko Ureno wiki ijayo Jumatano tarehe 15 Aprili.
Na Arsenal waliokuwa ugenini huko Spain wakipambana na Villareal wametoka suluhu ya 1-1.
Matokeo haya si mabaya sana kwa Arsenal kwani wakiepuka kufungwa au suluhu ya zaidi ya 1-1 basi watasonga mbele.

No comments:

Powered By Blogger