Sunday 29 June 2008



FAINALI: misuli v ustadi!


Bila shaka Euro 2008 imetupa utamu hasa baada ya kuuzoea ule uhondo wa LIGI KUU UINGEREZA iliyomalizika Mei. Kweli tumeshuhudia mechi 30 zilizojaa ufundi, ari, utata, vipaji na leo tupo kwenye mechi ya mwisho-FAINALI, kati ya Ujerumani na Uhispania.
Leo ni mashindano kati ya Nguvu asilia na Akili kichwani! Ni patashika ya Misuli ya Ujerumani na Ustadi wa Uhispania!
Ujerumani wakiongozwa na Meneja ‘kijana’ Joachim 'Jogi' Low, umri miaka 48, ambae hupenda kuvaa ‘kileo’ na Spain wana meneja ‘mzee’ Luis Aragones, miaka 69, ambae wengi humtambua ni mkorofi na haogopi kusema kitu chochote!
Meneja wa zamani wa Uingereza Graham Taylor ananena: "Kimkakati, ni vita kati ya mchezo wa pasi fupifupi na wepesi wa Spain dhidi ya mpira wa moja kwa moja wa Ujerumani ambao daima wao vita mbele tu!"
Graham Taylor anaongeza: "Spain wanajua kucheza aina moja ya mchezo tu! Kushambulia! Kiuchezaji wanafanana na Arsenal na hivyo ikiwa Ujerumani watawaachia waje kushambulia tu na kuwavizia kwa mashambulizi ya kushtukiza, Ujerumani watapotea! Nguvu ya Ujerumani ni mipira ya juu na mipira ya juu ni udhaifu mkubwa wa Spain!"

No comments:

Powered By Blogger