Friday 4 July 2008

BEKI WA USWISI AJIUNGA LIVERPOOL
Liverpool wamemsaini mlinzi wa Timu ya Taifa ya Switzerland Philipp Degen kutoka klabu ya Kijerumani Borussia Dortmund. Mchezaji huyo mwenye miaka 25 ni beki wa kulia na itabidi agombee namba hiyo na mabeki wengine wawili wa kulia Alvaro Arbeloa na Steve Finnan.
Degen amesaini mkataba wa miaka mine na alikuwa mchezaji wa akiba kwenye EURO 2008 iliyoisha hivi juzi.
CRESPO SASA RASMI NJE CHELSEA!
Mshambuliaji Hernan Crespo amehama rasmi Chelsea baada ya mkataba wa Muargentina huyo kuisha.
Crespo, umri miaka 33, alijiunga Chelsea 2003 na akapelekwa AC Milan kwa mkopo mwaka mmoja baadae. Akarudi tena Chelsea msimu wa 2005/06 na kuisaidia kunyakua Ubingwa wa LIGI KUU UINGEREZA.
Baada ya msimu huo akarudishwa tena kwa mkopo AC Milan na inasemekana sasa atasaini mkataba wa kudumu na Inter Milan baada ya Bosi wake wa zamani Jose Mourinho kuteuliwa Meneja wa Inter Milan
.

No comments:

Powered By Blogger