Saturday 5 July 2008

RUSHWA SERIE A ITALIA!
Wachezaji watano wa Serie A, LIGI YA JUU huko Italia, wameshtakiwa kwa kupanga matokeo ya mechi ambayo ilihusisha timu za Atalanta na timu iliyoshushwa daraja Livorno. Mashtaka hayo yanahusu mechi zote mbili za timu hizo za nyumbani na ugenini za msimu uliopita ulioisha mwezi Mei.
Mchezaji wa Atalanta Gian Paolo Bellini na aliekuwa Nahodha wa Livorno David Balleri wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga matokeo. Ndugu wawili na wachezaji wa Livorno Emanuele na Antonio Filippini pamoja na mchezaji mwingine wa timu hiyo Alessandro Grandoni wameshtakiwa kwa kosa la kutotoa taarifa kwa wahusika kuhusu maovu hayo.
Timu hizo zilitoka sare 1-1 tarehe 23 Decemba 2007 na mechi ya marudiano ya tarehe 4 Mei 2008 Atlanta walishinda 3-2.
Klabu zote hizo mbili zipo pia matatani mbele ya vyombo vya soka.
Soka ya Italia si ngeni kwa tuhuma za rushwa na kupanga matokeo mechi.
Mwaka 2006, Klabu maarufu za Lazio, Fiorentina na AC Milan zilinyang’anywa pointi kwa kupanga matokeo na Juventus wakashushwa daraja.

No comments:

Powered By Blogger