Sunday 29 June 2008

NAHODHA WA UJERUMANI HATIHATI KUCHEZA!
Michael Ballack aumia mazoezini!

Spain mfumo wawachanganya!
Nahodha wa Germany Michael Ballack yuko kwenye hatihati ya kutocheza Fainali ya Euro 2008 baada ya kupata maumivu mguuni na kusababisha akose mazoezi Ijumaa na Jumamosi.
Kuikosa mechi hii kwa Ballack, mwenye umri wa miaka 31, kutakuwa pigo kubwa kwa Ujerumani kwa kumkosa Nahodha wao na vilevile kwa Ballack binafsi kwani mwaka 2002 aliikosa Fainali ya Kombe la Dunia alipofungiwa kucheza kutokana na kadi.
Kwa upande wa Spain, zaidi ya kumkosa mfungaji bora wa EURO 2008, David Villa, ambae ni majeruhi na hachezi fainali, timu haina tatizo kubwa isipokuwa kuamua mfumo upi watautumia- ama 4-5-1 ukimfanya Fabregas awe kati pamoja na viungo wengine wanne huku Fernando Torres akiwa mshambuliaji pekee au wacheze 4-4-2 na hivyo Fabregas awe benchi na timu iwe na washambuliaji wawili yaani Torres na Daniel Guiza.
Huo ndio mtihani unaoikabili Spain ambayo haijachukua kombe lolote kubwa tangu mwaka 1964 waliponyakua Kombe la Mataifa ya Ulaya.
USO KWA USO
Germany na Spain zimeshakutana mara 19 huku Wajerumani wakishinda mara 8 na Spain mara 5.
Katika Kombe la Dunia na Kombe la Mataifa Ulaya washakutana mara 5 Ujerumani ikishinda mara 3 na Spain mara 1 tu.
Mara ya mwisho timu hizi kukutana ni kwenye mechi ya kirafiki Februari 2003 na Spain walishinda 3-1.

No comments:

Powered By Blogger