Sunday 29 June 2008

REFA ROBERTO ROSETTI- Mtaliano atakaechezesha FAINALI!
Germany wanamkumbuka Refa huyu hasa baada ya kipigo kitakatifu walichokipata kwenye mechi ya kirafiki tarehe 28 April 2004 walipobamizwa na Romania 5-1.
Hata hivyo Roberto Rosetti alikuwa Refa hivi karibuni tu wakati Germany waliposhinda ugenini 2-1 dhidi ya Czech Republic kwenye mechi za mitoano ya awali kuwania nafasi za kuingia Fainali za EURO 2008.
Spain nao wana hisia tofauti na Mtaliano huyu.
Roberto Rosetti alikuwa Refa kwenye Kombe la Dunia 2006 Spain walipofungwa 3-1 na France katika Robo Fainali. Kwenye mechi za mitoano ya awali kuwania nafasi za kuingia Fainali za EURO 2008 Roberto Rosetti alikuwa mwamuzi kwenye mechi ya Spain walipowatoa Sweden 3-0.
Leo, Roberto Rosetti atawapa bahati nani?

No comments:

Powered By Blogger