Friday 4 July 2008



UHAMISHO LIGI KUU.................................


Middlesbrough wamemsajili Mshambuliaji wa Sparta Rotterdam ya Uholanzi Marvin Emnes kwa Pauni za Kiingereza milioni £3.2m.
Emnes, miaka 20, amesaini mkataba wa miaka minne baada ya kukubaliana na Middlesbrough malupulupu binafsi na kufaulu vipimo vya kiafya. Mchezaji huyo aliezaliwa mjini Rotterdam huichezea Timu ya Taifa ya Uholanzi ya vijana wa chini ya miaka 21 na msimu uliopita aliteuliwa Mchezaji Bora wa Klabu yake Sparta Rotterdam
.

Galatasaray wanadai wamemsaini Harry Kewell ingawa Klabu yake ya Liverpool haijathibitisha. Tovuti ya Klabu hiyo ya Kituruki imesema Kewell, miaka 29, amesaini mkataba wa miaka mitatu baada ya Meneja wa Liverpool Rafael Benitez kukataa kumuongezea muda.
Kewell yupo Liverpool kwa miaka mitano sasa ingawa muda mwingi ni majeruhi.

Fulham wamempata mlinzi kutoka Finland aitwae Toni Kallio, umri miaka 29, kwa mkataba wa kudumu wa miaka miwili baada ya kuja hapo Januari mwaka huu kwa mkopo. Mchezaji huyo alitokea Klabu ya Uswisi BSC Young Boys.





No comments:

Powered By Blogger