Sunday 29 June 2008


Wenger ataka Ronaldo abaki!
-Na Adebayor adengua!
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini ni muhimu kwa Manchester United kuhakikisha Cristiano Ronaldo anabaki Old Trafford ili kupinga juhudi zisizo halali za Real Madrid kumchukua.
Wenger ameusifia msimamo wa Man United wa kukataa kuzungumza na mtu yeyote kuhusu uhamisho wa Ronaldo kwa sababu anataka LIGI KUU UINGEREZA iimarike zaidi na zaidi. Vilevile amesisitiza Real Madrid wamevunja sheria kwa kujaribu kumrubuni Ronaldo.
Alipoulizwa kama yeye binafsi anataka Ronaldo ahamie Spain alijibu:"Hapana, hapana hata kidogo! Mie nataka kuwe na msimamo. Nataka LIGI KUU UINGEREZA iwe bora duniani na nataka nijue nikiwafunga Man United, nikiwafunga Chelsea, basi nazifunga timu bora duniani!’’
Wakati huo huo, Arsene Wenger amesisitiza Emmanuel Adebayor atabaki Arsenal msimu ujao kwa sababu ana mkataba na klabu hiyo. Adebayor mwenyewe na vyombo vya habari lukuki vimekuwa vikisema anahama ingawa haijulikani waziwazi anahamia wapi.

No comments:

Powered By Blogger