Sunday 25 January 2009

KOMBE LA FA: Bila shaka Everton watalia: OOOHHH REFA!!!!
Liverpool 1 Everton 1

Wakicheza ugenini, nyumbani kwa Watani wao wa Jadi Liverpool Uwanjani Anfield, Everton walionekana dhahiri kukandamizwa na Waamuzi wa mechi hiyo wakiongozwa na Refa Steve Bennet.
Dakika ya 5 tu ya mchezo walinyimwa penalti ya wazi pale Kiungo wa Liverpool Xabi Alonso alipomkwatua Steven Pienaar.
Lakini Mwamuzi alishindwa kulikataa goli safi na la wazi la Mlinzi wa Everton Joleon Lescott aliefunga kwa kichwa kufuatia kona ya Steven Pienaar dakika 27 na kumkuta Tim Cahill aliepiga kichwa kilichokuwa kinaenda wavuni lakini Lescott akamalizia na kujihesabu yeye ndie mfungaji.
Mpaka mapumziko Liverpool 0 Everton 1.
Kipindi cha pili Liverpool huku wakibebwa na Waamuzi walijitutumua na kusawazisha dakika ya 54 kupitia mkombozi na Nahodha wao Steven Gerrard.
Hii ni mara ya pili kwa Liverpool kushindwa kumfunga Mtani wake hapo kwake Anfield ndani ya wiki moja baada ya kutoka droo ya 1-1 kwenye mechi ya LIGI KUU Jumatatu iliyokwisha.
Sasa timu hizi zitarudiana huko Goodison Park nyumbani kwa Everton wiki ijayo tarehe 4 Februari 2009 ili kuamua ni nani kati yao ataingia Raundi ya 5 ya Kombe la FA.

No comments:

Powered By Blogger