Tuesday 27 January 2009

UHAMISHO: Klabu za LIGI KUU England:

Dirisha la Uhamisho wa Wachezaji linafungwa tarehe 1 Februari 2009 na Klabu mbalimbali zipo kwenye harakati za kuuza na kununua Wachezaji.
Baadhi ya makubaliano yaliyofanyika ni kama ifuatavyo:

Chimbonda arudi tena Tottenham!!

Pascal Chimbonda, Beki mwenye umri wa miaka 29, amerudi tena Tottenham kutoka Sunderland ambako alicheza mechi 16 tangu aende huko kutoka Tottenham mwezi Agosti mwaka jana.
Chimbonda, ambae pia ameshachezea Timu ya Taifa ya Ufaransa, alikwenda England kuchezea Wigan akitokea Klabu ya Bastia ya Ufaransa na mwezi Agosti, 2006 alijiunga na Tottenham.

Tottenham wamsaini Kipa Cudicini toka Chelsea!

Kipa Carlo Cudicini, miaka 35, amehamia Tottenham kutoka Chelsea kwa uhamisho wa bure baada ya mkataba wake kukaribia kuisha.
Cudicini alijiunga Chelsea mwaka 1999 akitokea Castel de Sangro ya Italia na ameshaidakia Chelsea mechi 208 lakini tangu Kipa Petr Cech aingie Chelsea 2004, Cudicini amekuwa hana namba.
Hata huko Tottenham atapata ushinda mkubwa kwani kuna Makipa Heurelho Gomes, anaesifika sana kwa kutoa maboko na chipukizi Ben Alnwick.

West Ham wamchukua Nsereko aliezaliwa Uganda!!

Savio Nsereko, kijana wa miaka 19 mzaliwa wa Uganda ingawa sasa ni raia wa Ujerumani, amejiunga na West Ham akitokea Klabu ya Italia ya Serie B Brescia kwa dau la Pauni Milioni 7 na nusu.
Nsereko huchezea Timu ya Taifa ya Ujerumani ya Vijana wa chini ya miaka 19.

Wigan wamnunua Straika toka Colombia!

Mshambuliaji mwenye umri wa miaka 23 aitwae Hugo Rodallega amejiunga na Wigan kutoka Klabu ya Mexico Necaxa kwa ada ya Puni Milioni 4 na nusu na mkataba wa miaka mitatu na nusu.
Rodallega pia yumo Timu ya Taifa ya Colombia ambayo ameichezea mechi 21.
Kujiunga kwa Rodallega Wigan kuna nia ya kujiimarisha baada ya Mshambuliaji wao staa Emile Heskey kuhamia Aston Villa wiki iliyokwisha.
Safu hiyo ya mashambulizi pia imeongezwa nguvu baada ya Wigan kumchukua Mmisri Mido kwa mkopo kutoka Middlesbrough.

LIGI KUU kuendelea leo usiku!!!

Baada ya mshikemshike wa FA CUP, LIGI KUU England inarudi tena ulingoni leo usiku kwa ratiba ifuatayo:

Jumanne, 27 Januari 2009
[saa 4 dak 45 usiku]

Sunderland v Fulham

West Brom v Man U

[saa 5 usiku]
Portsmouth v Aston Villa
Tottenham v Stoke

Jumatano, 28 Januari 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Chelsea v Middlesbrough
Man City v Newcastle
Wigan v Liverpool
[saa 5 usiku]
Blackburn v Bolton
Everton v Arsenal
West Ham v Hull

Jumamosi, 31 Januari 2009
[saa 9 dak 45 mchana]
Stoke v Man City
[saa 12 jioni]
Arsenal v West Ham
Aston Villa v Wigan
Bolton v Tottenham
Fulham v Portsmouth
Hull v West Brom
Middlesbrough v Blackburn
[saa 2 na nusu usiku]
Man U v Everton

Jumapili, 1 Februari 2009
[saa 10 na nusu jioni]
Newcastle v Sunderland
[saa 1 usiku]
Liverpool v Chelsea

No comments:

Powered By Blogger