Thursday 29 January 2009

Liverpool wakwaa kisiki, Chelsea achupa juu yake, Arsenal mwendo mdebwedo lakini Man U bado juu, pointi 2 mbele, mechi moja mkononi!!!!!

Mabingwa Manchester United sasa wako juu ya Wapinzani wao Chelsea na Liverpool kwa pointi 2 na bado wana mechi moja mkononi kufuatia matokeo ya mechi za juzi na jana.
Juzi, Man U waliwachabanga West Brom Albion 5-0 na jana Liverpool walikwaa kigingi pale walipotoka sare 1-1 na Wigan huku Chelsea akiifunga Middlesbrough 2-0.
Liverpool walifunga bao lao kupitia Yossi Benayoun lakini Mmisri Mido, akicheza mechi yake ya kwanza kwa Wigan tangu ahamie hapo kwa mkopo toka Middlesbrough, alisawazisha kwa penalti dakika ya 84.
Nae Salomon Kolou aliifungia Chelsea mabao 2 na kuwapa ushindi wa 2-0 dhidi ya Middlesbrough na kuwafanya Chelsea kuipita Liverpool katika msimamo wa Ligi na kuwa wa pili nyuma ya Man U na sasa wako pointi 48 sawa na Liverpool lakini Chelsea yuko mbele kwa kuwa na tofauti ya magoli bora wote wakiwa wamecheza mechi 23.
Man U yuko kileleni akiwa na pointi 50 kwa mechi 22.
Aston Villa walijikita nafasi ya 4 kwa ushindi wa bao 1-0 walipoifunga Portsmouth nyumbani kwake juzi na sasa wana pointi 47 kwa mechi 23 wakiwa mbele ya Arsenal kwa pointi 5.
Nao Arsenal sasa inaelekea wanaaga rasmi kuwania Ubingwa kwani jana nusura wafungwe pale walipochomoa kigoli dakika za majeruhi dhidi ya Everton.
Everton walipachika bao lao kupitia Tim Cahill dakika ya 61 aliefunga kwa kichwa kama kawaida yake lakini Robin van Persie aliisawazishia Arsenal kwa shuti kali kwenye dakika ya 91.
Sasa Arsenal wamecheza mechi 23 na wana pointi 42 huku Everton wako nyuma ya Arsenal wakiwa na pointi 37 kwa mechi 23 pia.

MECHI ZIFUATAZO:


Jumamosi, 31 Januari 2009

[saa 9 dak 45 mchana]

Stoke v Man City

[saa 12 jioni]

Arsenal v West Ham
Aston Villa v Wigan
Bolton v Tottenham
Fulham v Portsmouth
Hull v West Brom
Middlesbrough v Blackburn

[saa 2 na nusu usiku]

Man U v Everton

Jumapili, 1 Februari 2009
[saa 10 na nusu jioni]

Newcastle v Sunderland

[saa 1 usiku]

Liverpool v Chelsea

No comments:

Powered By Blogger