Friday 30 January 2009

MACHO YAKO KWA Liverpool v Chelsea Jumapili, Mtaalam anena atakaefungwa : 'USIKU MWEMA KWA UBINGWA!!!'

Timu zote za LIGI KUU England zitacheza Jumamosi na Jumapili za Wikiendi hii, lakini ukweli ni kwamba macho ya Washabiki siku ya Jumamosi yatakuwa kwa Mabingwa Manchester United wakiwakaribisha Everton Old Trafford na wengi wanaamini Man U watashinda na kuwa pointi 5 mbele ya Liverpool na Chelsea wanaopambana wenyewe Jumapili huko Anfield, mjini Liverpool.
Mtaalam mmoja anaekubalika vizuri huko England amesema:
'Yeyote kati ya Liverpool au Chelsea akifungwa tu hiyo Jumapili basi atakuwa ametamka 'Usiku Mwema' kwa Ubingwa wa LIGI KUU! Nategemea Man U itaifunga Everton siku ya Jumamosi na hivyo kuwa pointi 5 mbele ya Chelsea na Liverpool. Ni muhimu mmoja ashinde ili awe anaifukuza na kuweka presha kwa Man U lakini atakaefungwa ana kazi kubwa sana ya kupigana na Aston Villa anaekuja kama mbogo kugombea nafasi ya 3! Aahh, Arsenal, naamini wataibuka tu!!'

No comments:

Powered By Blogger