Friday 30 January 2009

Vidic kuikosa mechi ya kwanza na Inter Milan!!

Beki mahiri wa Manchester United, Nemanja Vidic, amefungiwa mechi moja na FIFA baada ya kupewa Kadi Nyekundu kwenye Fainali ya Kombe la Dunia la Klabu kati ya Man U na LDU Quito mwezi Desemba ambayo Man U waliibuka Mabingwa wa Dunia kwa ushindi wa bao 1-0, bao alilofunga Wayne Rooney.
Adhabu hii, ambayo haiwezi kukatiwa rufaa, itasababisha Vidic kuikosa mechi dhidi ya Inter Milan itakayochezwa Februari 24 huko San Siro kwenye kinyang'nyiro cha UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Timu hizo zitarudiana Machi 11, huko Old Trafford nyumbani kwa Man U.
Vidic pia amepigwa faini ya Pauni 2,985.

NANI KASEMA???????

'Kipindi cha pili kilikuwa ni uchizi mtupu na gemu ikiwa ya kichizi huwezi kuidhibiti! Kwa nini ilikuwa ya kichizi? Kwa sababu ilikuwa ya kichizi!!!'
Rafa Benitez, Meneja wa Liverpool aliepata uchizi baada ya kutoka droo 1-1 na Wigan na kuwaacha Man U kileleni!.

'Hii ni Klabu ya Soka iliyojengwa na sijui na nani na na namna gani!! Ni mchanganyiko wa Wachezaji wa kushangaza sana!! Inatisha!!'
Harry Redknapp akiishangaa Timu yake mbovu ya Tottenham aliyoirithi kama Meneja mpya.

'Nadhani kuna watu wanahitaji kwenda Kanisani Jumapili kuungama!!'
Mshambuliaji wa Reading Stephen Hunt akiituhumu Klabu yake kwa kusema uongo kuwa hakuna Timu inayotaka kumnunua.

'Viva Da Silva, Viva Da Silva, wakiwa Uwanjani, humjui Nani ni Nani, Viva Da Silva!'
Mashabiki wa Manchester United wakiimba Old Trafford baada ya kumuona Pacha Mwenza wa Rafael Da Silva aitwae Fabio Da Silva, ambao wamefanana mno na huwezi kuwatofautisha, akicheza mechi yake ya kwanza kwa Timu hiyo dhidi ya Derby County kwenye Kombe la Carling.

'Kaka, popote ulipo,
Umeisikia Man City?
Usiende huko,
Utalia machozi,
Hawajachukua Kikombe Miaka 33'
Mashabiki wa Wigan wakiwaimbia na kuwatambia Manchester City timu zao zilipokutana huku wakimuonya Kaka wa AC Milan na Brazil.

No comments:

Powered By Blogger