Wednesday 28 January 2009

ROBINHO MBARONI KWA TUHUMA ZA KUBAKA!!

Robinho, ambae wiki iliyokwisha alitoroka kwenye kambi ya Timu yake Manchester City iliyokuwa imepigwa huko Spain na kutimka kwao Brazil na kusababisha Klabu yake kumpiga faini na kumpa onyo kali, sasa yuko mikononi mwa Polisi wanaouchunguza uhalifu wa shambulio la ngono lilotokea Januari 14 kwenye naiti klabu.
Msemaji wa Polisi wa West Yorkshire amethibitisha kukamatwa kwa mtu mmoja anaesadikiwa ni Robinho ingawa amesema mtu huyo amekanusha tuhuma hizo na ametoa ushirikiano na yuko nje kwa dhamana.


ENGLAND YAOMBA RASMI KUANDAA FAINALI KOMBE LA DUNIA 2018

FA ya England imewasilisha ombi rasmi kwa FIFA la kuomba kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia la mwaka 2018.
Tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi ya kuwa mwenyeji wa Kombe hilo ni tarehe 2 Februari.
England walikuwa wenyeji wa Fainali hizo mwaka 1966 na ndio safari pekee waliyotwaa Kombe hilo.
Mpaka sasa ni Spain na Portugal, kwa pamoja, na, Holland na Belgium, pia kwa pamoja ndio waliowasilisha maombi ya kuwa wenyeji.
Nchi binafsi zilizoomba ni Urusi, Australia na Qatar huku China, Japan na USA zinasadikiwa zitaomba.
Sharti kubwa la kuwa Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia ni kuwa na Viwanja si chini ya 12 vyenye uwezo wa kuchukua Watazamaji 40,000 kila kimoja n Fainali ichezwe kwenye Uwanja wa Watazamaji 80,000.
Fainali za Kombe la Dunia za 2010 zitafanyika Afrika Kusini na za 2014 zitakuwa Brazil.
FIFA itatangaza Wenyeji wa Fainali za 2018 na 2022 mwezi Desemba 2010.

HATMA YA VIDIC KUPEWA KADI NYEKUNDU FAINALI YA KLABU BINGWA YA DUNIA NI IJUMAA!!!

Beki wa Manchester United, Nemanja Vidic, atajua siku ya Ijumaa nini kitamkuta kama adhabu ya nyongeza baada ya kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu kwenye Fainali ya Kombe la Dunia la Klabu mwezi Desemba huko Japan katika pambano la Man U na LDU Quito wakati alipompiga kiwiko Claudio Bieler.

FIFA imelipeleka suala hilo kwa UEFA kwani Manchester United walikuwa wanaiwakilisha UEFA kwenye mashindano hayo na UEFA imetamka itasikiliza kesi hiyo na kutoa uamuzi siku ya Ijumaa.

Man U watakuwa wanaomba UEFA ichukue uamuzi kama walioufanya miaka miwili iliyopita pale walipoamua kutochukua hatua yeyote ya ziada kwa Mchezaji wa AC Milan Kakha Kaladze aliepewa Kadi Nyekundu kwenye Fainali za Klabu Bingwa ya Dunia na FIFA wakaisukumia UEFA kutoa adhabu zaidi lakini Mchezaji huyo hakupewa adhabu nyingine yeyote na UEFA.

No comments:

Powered By Blogger