Sunday 25 January 2009

DRO YA RAUNDI YA 5 YA KOMBE LA FA KUFANYIKA LEO USIKU.

Dro ya kuamua Timu zipi zinakutana kwenye Raundi ya 5 ya FA Cup ambayo itajumuisha Timu 16 itafanyika leo usiku baada ya mechi ya Raundi ya 4 ya Kombe hili kati ya Liverpool na Everton itakayoanza saa 1 usiku [bongo taimu].
Mechi nyingine ya Raundi ya 4 inayochezwa leo ni kati ya Cardiff na Arsenal inayoanza saa 10 na nusu jioni [bongo taimu].
Mechi nyingine za Raundi ya 4 inazobidi zirudiwe baada ya kutoka suluhu hapo jana ni kama ifuatavyo:

Jumanne, 3 Februari 2009
Burnley v West Brom
Jumatano, 4 Februari 2009
Aston Villa v Doncaster
Blackburn v Sunderland
Nottingham Forest v Derby

Washindi wa mechi hizo za marudiano, pamoja na Washindi wa mechi 2 za leo, watajumuika na Timu zilizofuzu kuingia Raundi ya 5 zifuatazo: Manchester United, Hull City, West Ham, Sheffield United, Swansea City, Chelsea, Coventry City, Fulham, Watford na Middlesbrough.
Mechi hizi za Raundi ya 5 zitachezwa tarehe 14 Februari 2009.

No comments:

Powered By Blogger