Sunday 25 January 2009

Mechi ya jana ya FA CUP kati ya Hull City na Millwall yatawaliwa na fujo za mashabiki wa Millwall!!! Kikosi cha Polisi wa Kuzuia Fujo chaingilia na kuwakamata Washabiki 12!!!

Katika mechi ya jana kati ya Hull City na Millwall ya Raundi ya 4 ya Kombe la FA ambayo Hull aliibuka na ushindi wa mabao 2-0, vurugu na fujo kubwa ziliibuka kabla ya mechi kuanza na hata wakati mechi ikiendelea hasa kwenye jukwaa walilokaa Washabiki wa Millwall ambao ndio walikuwa uwanja wa ugenini.
Kizaazaa hicho hakijawahi kuonekana kwenye mechi za Soka England kwa miaka sasa.
Ilibidi Kikosi Maalum cha Polisi wa Kuzuia Fujo waliovalia rasmi kwa mapambano kuitwa na waliangusha mkong'oto mkubwa na kuwakamata Mashabiki 12 wa Millwall na uchunguzi wa video unaendelea ili kuwakamata wahusika wengine.
Klabu ya Hull City iko mbioni kudai fidai kwa kuharibiwa uwanja wao ambao viti viling'olewa, vyoo kuvunjwa na mali zao nyingi kuharibiwa.
Mechi ilihudhuriwa na Watazamaji zaidi ya 18,000.

No comments:

Powered By Blogger