Saturday 24 January 2009

Man U watinga Raundi ya 5 FA Cup: Man U 2 Tottenham 1

Ndani ya Uwanja wao Old Trafford, Manchester United wamewabwaga wapinzani wao watakaokutana nao kwenye Fainali ya Carling Cup Machi 1, 2009, Tottenham, kwa mabao 2-1 na hivyo kuwatoa kwenye Kombe la FA.
Magoli yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza huku Tottenham wakitangulia kufunga dakika ya 5 tu kupitia Mrusi Roman Pavyluchenko kufuatia krosi ya Tom Hudllestone.
Man U wakafunga bao mbili za haraka ndani ya dakika moja kupitia Paul Scholes dakika ya 35 na Dimitar Berbatov dakika ya 36.
Kivutio kwenye mechi hii ni Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, kuamua kumchezesha kwa mara ya kwanza pacha mwenza wa Rafael aitwae Fabio kama Beki wa pembeni kushoto na kabla ya kuumia alicheza vizuri sana na kushangiliwa sana na Watazamaji.
Rafael na Fabio da Silva ni vijana wa miaka 18 wanaotoka Brazil.
Rafael huwa anacheza Beki wa pembeni kulia.
Man Utd: Foster, O'Shea, Neville, Vidic, Fabio Da Silva (Eckersley 53), Welbeck (Fletcher 86), Carrick, Scholes, Ronaldo (Tosic 72), Berbatov, Tevez.
Akiba hawakucheza: Kuszczak, Giggs, Possebon, Chester.
Kadi: Vidic, Tevez.
Magoli: Scholes 35, Berbatov 36.
Tottenham: Alnwick, Gunter, Corluka, Dawson, Assou-Ekotto, Bentley (Defoe 72), Huddlestone, Zokora, Bale (Taarabt 67), Modric (Giovani 46), Pavlyuchenko.

Akiba hawakucheza: Gomes, Gilberto, Rocha, Dervite.
Goli: Pavlyuchenko 5.
Watazamaji: 75,014
Refa: Peter Walton


MECHI ZA JUMAPILI 25 JANUARI 2009 KOMBE LA FA:

Cardiff v Arsenal [saa 10 na nusu jioni]

Liverpool v Everton [saa 1 usiku]

No comments:

Powered By Blogger