Saturday 24 January 2009

NI WIKIENDI YA KOMBE LA FA!

Wikiendi hii kutakuwa hamna mechi za LIGI KUU England na badala yake Vilabu vya Madaraja mbalimbali vitaingia dimbani kuwania nafasi za kusonga michuano ya Kombe hili.
Ratiba ni kama ifuatavyo:
Jumamosi, 24 Januari 2009 Mechi za Kombe la FA [mechi zote saa 12 jioni saa za bongo isipokuwa zilizotajwa]
Chelsea v Ipswich
Doncaster v Aston Villa
Hartlepool v West Ham [saa 9 dak 40]
Hull v Millwall
Kettering v Fulham
Man U v Tottenham [saa 2 na robo usiku]
Portsmouth v Swansea
Sheffield United v Charlton
Sunderland v Blackburn
Torquay v Coventry Watford v Crystal Palace
West Brom v Burnley
Wolverhampton v Middlesbrough
Jumapili, 25 Januari 2009 Mechi za Kombe la FA
Cardiff v Arsenal [saa 10 na nusu jioni]
Liverpool v Everton [saa 1 usiku]

Villa wamnunua Emile Heskey kutoka Wigan, Mido aenda Wigan kwa mkopo!

Aston Villa wamemsaini Emile Heskey kutoka Wigan kwa dau la Pauni Milioni 3.5 na wakati huohuo Mchezaji wa Kimataifa wa Misri Mido amechukuliwa na Wigan kwa mkopo kutoka Middlesbrough hadi mwisho mwa msimu huu.
Msimu huu Mido amefunga mabao manne katika mechi 13 alizochezea Middlesbrough.
Mido anakuwa Mshambuliaji wa pili kutua Wigan kufuatia kusainiwa kwa Hugo Rodallega kutoka Colombia kwa ada ya Pauni Milioni 4.5.

No comments:

Powered By Blogger